Waandamanaji wanapinga hatua ya serikali kuondoa ruzuku ya mafuta
Polisi
nchini Sudan wamewatifulia gesi ya kutoa machozi waandamanaji katika
Mji Mkuu
Khartoum, huku wengi wakiendelea kukasirishwa na kuondolewa
kwa ruzuku ya mafuta.
Walioshuhudia maandamano hayo walisema kuwa
waandamanaji waliteketeza jengo moja la Chuo
Kikuu na vituo kadhaa vya
petroli. Pia waliziba njia kuu ya kuelekea uwanja wa ndege.
Watu wawili wameuawa tangu maandamano hayo kuanza Jumatatu wakati Serikali ilipotangaza
kuondolewa kwa ruzuku ya mafuta.
Hatua hiyo imefikiwa katika juhudi za serikali kuongeza mapato ya Serikali.
Hata hivyo waandishi wa habari hapo mjini
wanasema kuwa hatua hiyo imewaathiri zaidi watu wa
mapato ya chini na
kuzusha Serikali kuchukiwa na raia wa kawaida.
Duru zinasema kuwa watu watatu wamefariki
kutokana na ghasia hizo. Waziri wa elimu naye
amesema kuwa shule ziliko
katika mji mkuu zitasalia kufungwa hadi Septemba tarehe 30.
Kwa mujibu wa shirika la AFP, watumijai wa
mtandao wa internet wanasema kuwa huduma
zimekatizwa ingawa haijulikani
ikiwa ni hatua ya serikali kudhibiti mawasiliano au ilitokana na
hitilafu za kimitambo.
Serikali ilitangaza Jumatatu hatua zaidi za
kupandisha bei ya mafuta baada ya kusitisha ruzuku
kwa muda katika
juhudi za kuleta mageuzi ya kiuchumi nchini humo.
Mnamo siku ya Jumanne waandamanaji waliteketeza ofisi za chama tawala,mjini Omdurman.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni