Jumapili, 8 Septemba 2013

Tokyo yasherehekea kutuzwa Olimpiki 2020

Watoto wanaoneshana habari za magazeti kuwa Tokyo imechaguliwa kuandaa 2020 Olympics

Tokyo imekuwa ikisherehekea kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa michezo ya Olimpiki ya mwaka wa 2020.
Mji mkuu wa Japan uliishinda kwa urahisi miji ya Istanbul na Madrid.
Tangazo hilo lilotolewa na rais anayeondoka wa kamati ya kimataifa ya michezo ya Olympiki Jacques Rogge lilishangiliwa sana mjini Tokyo.
Tokyo ni mji wa tano ambao utakuwa umeandaa Olimpiki mara mbili.
Mwandishi wa BBC amesema kuwa mji huo ulijitembeza vyema katika siku ya mwisho ya kampeni lakini piya ulionekana kuwa thabiti kifedha na kiusalama
Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe, aliiambia kamati ya Olimpiki, IOC, kwamba matatizo ya miyonzi ya nuklia katika kinu cha nishati cha Fukushima hayataathiri michezo mjini

Hakuna maoni: