Jumatatu, 28 Oktoba 2013

AFRIKA NA MATUKIO KATIKA PICHA

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/28/131028123736__70679408_01_zim_jacaranda2_ap.jpg
Washidani katika mashindano ya mwanadada mrembo zaidi ya Miss Jacaranda nchini Zimbabwe wakionyesha hapa viatu vyao tayari kwa kutembea kwa madaha ukumbini
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/28/131028123749__70679410_02_tanzania_afp2.jpg 
Mjini Moscow Miss Tanzaia 2013 Betty Omara hapa anaonekana akirembwa kabla ya kupigwa picha. Shindano la mwanamke mrembo zaidi ulimwenguni litafanyika nchini Urusi mwezi Novemba ,9
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/28/131028130609__70694968_nigeria_fashion_afp.jpg
Hapa wanamitindo wa kiume wakiwa mjini Lagos wakishiriki onyesho la mitindo 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/28/131028123801__70694745_04_nigeriaz_breakdance_afp.jpg
Vijana wanadansi wa Nigeria wanaojulikana kama Space Unlimited wanashiriki mashindano ya kimataifa ya wakali wa Breakdance nchini Ujerumani siku ya Jumamosi
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/28/131028130646__70694972_somalia_afp.jpg
Siku ya Alhamisi kijana huyu alionekana mjini Mogadishu akiwabeba Samaki kutoka baharini katika eneo la Hamarweyne, si mavuno hayo?
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/28/131028124004__70694817_09_cameroon_pope_ap.jpg
Papa Francis hapa anaonekana akiongea na Chantelle Biya mke wa Rais wa Cameroon wakati alipokutana naye mjini Vatican siku ya Ijumaa
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/28/131028124025__70694857_11_tunisia_heart_ap.jpg
Mwanamke huyu alikuwa nchini Tunisia na hapa anaonekana akiweka alama ya moyo kwenye ngao ya polisi wakati wa maandamano siku ya Jumatano mjini Tunis
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/28/131028123933__70694796_07_kenya_westgate_afp.jpg
Hii ni DVD yenye filamu kuhusu shambulizi la Westgate inayouzwa na mchuuzi mjini Nairobi. Watu 67 waliuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa kwenye mashambulizi ya kigaidi dhidi ya jengo la Westgate mwezi jana. Kundi la Alshabaab lilikiri kufanya shambulizi hilo. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/28/131028123918__70694794_06_kenya_soldiers_ap.jpg
Hawa ni wanajeshi wanawake wa Kenya wakiwa katika uwanja wa kitaifa wa Nyayo wakati wa sherehe za kuwakumbuka mashujaa wa Kenya 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/28/131028130241__70694877_12_morcco_afp.jpg
Wacheza soka wa Morocco, wanasherehekea baada ya kuingiza bao katika mechi waliyoshinda dhidi ya Croatia siku ya Ijumaa kwa mababo 3-1 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/28/131028130541__70694910_14_madagascarbrooms_reuters.jpg
Mjini Antananrivo, kijana huyu anaonekana akiuza vifagio 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/28/131028130553__70694942_15_mada_bananas_ap.jpg
Katika mji huohuo, mtoto huyu alipigwa picha akiwa nyuma na ndizi zilizo katika kibanda cha babake cha kufanyia biashara kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/28/131028130620__70694970_liberia_ivory_afp.jpg
Watu mjini Zwedru Liberia, wanapeperusha bendera ya Ivory Coast, huku rais wa nchi hiyo Alassane Ouattara na mwenzake wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf wakihudhuria mkutano wa viongozi wa kijamii siku ya Jumamosi. Liberia ni nyumbani kwa wakimbizi zaidi ya 62,000 wa Ivory Coast waliotoroka ghasia za baada ya uchaguzi mwaka 2010

USIKOSE WIKI IJAO

Hakuna maoni: