Maandamano ya watu waliokuwa
wanaunga mkono walimu wanaodai mishahara bora zaidi nchini Brazil,
yamegeuka na kuwa makabiliano kati yao na polisi katika miji ya Rio de
Janeiro na Sao Paulo.
Mji wa Rio ulikuwa umesongamana watu zaidi ya 10,000 wakiandamana kwa amani .
Lakini usiku ulipoingia, waandamanaji kadhaa
walirusha mabomu ya moto katika majengo ya serikali nao polisi
wakawarushia gesi ya kutoa machozi ili kuwatawanya.
Maandamano sawa na hayo yalitokea mjini Sao
Paulo na pia kusababisha ghasia na makabiliano makali kati ya polisi na
waandamanaji hao waliokuwa wamefunika nyuso zao na kuvamia benki.
Hali ya usalama nchini Brazil, ni changamoto
kubwa ambayo huenda ikajitokeza zaidi wakati wa kombe la dunia mwaka
2014 na michezo ya olimpiki mwaka 2016 .
Maandamano ya hivi karibuni yalidumu kwa masaa kadhaa na yalikuwa salama mwanzoni.
Lakini usiku ulipoingia ghasia zikazuka huku
waamdanamanaji wakiteketeza majengo ya serikali na wengine kuvamia benki
na kuvunja mashine za pesa. Baadhi ya benki ziliteketezwa.
Waandamanaji hao pia waliiba viti kwenye benki na kuvitumia kama vizuizi kati yao na polisi.
Polisi walilazimika kutumia gesi ya kutoa
machozu kurejesha utulivu.Walimu wamekuwa wakidai nyongeza ya mishahara
kwa miezi kadhaa sasa.
Takriban watu 50,000 walikadiriwa kuandamana ili
kuwaunga mkono walimu kabla ya ghasia kuzuka lakini polisi waliweza tu
kuthibitisha watu 10,000 walishiriki maandamano hayo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni