Glenna Gordon anasema: "harusi za Nigeria ni sawa na ilivyo nchi yenyewe
ya Nigeria: Kubwa, Zenye kelele na zenye furaha tele. Muziki pia ni wa
sauti ya juu na chakula ni kizuri sana. Hakuna kilicho kimya Nigeria na
hiyo bila shaka ni kweli ya harusi. ''
''Baadhi ni kubwa zilizogharimu pesa nyingi na nyengine ni za
kufurahisha,'' anasema mpiga picha huyo ambaye amefanya kazi katika
maeneo mengi ya Afrika.
Licha ya hali, kila mtu hujitosa uwanjani akiwa amevalia mavazi yake mazuri zaidi
"wageni kwenye harusi hizo huvalia vyema tu kama bibi harusi. Nyingi ya
harusi hizo pia huwa na watu waliovalia mfano wa mavazi ya nyumbani au
aso-ebi katika lugha ya Yoruba, moja ya lugha maaruufu wanazoongewa watu
katika maeneo ya Kusini.''
"marafiki wa bibi harusi wote huvalia nguo za kufanana, marafiki za
mamake huvalia nguo tofauti na marafiki za mume pia hufanya hivyo.
''Kutumia simu yangu ya iPhone ilinisaidia sana kwa sababu kutumia
kamera kubwa inaweza kuleta kuzuizi kati ya mwenye kupigwa picha na
kamera''
Nilitaka kitu binafsi kuwezesha wenye kupigwa picha kukutana na wageni
na kuwapiga picha wakiwa katika mazingira yale ya sherehe.
Unaweza kuona picha zaidi za Gordon kwenye istaghram yake @glennagordon.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni