Alhamisi, 17 Oktoba 2013

YALIYOJILI AFRIKA WIKI HII

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/14/131014090720_lampedusa_kids_976x549_bbc_nocredit.jpg
Majeneza ya watoto waliokuwa miongoni mwa watu waliokufa maji katika kisiwa cha Lampedusa 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/14/131014090830_polisi_vurugu_976x549_bbc_nocredit.jpg
Mnamo Jumanne vikosi vya usalama katika mji mkuu wa Guinea-Bissau wanamlinda mwanamume raia wa Nigeria, kutokana na ghadhabu ya raia wa nchi hiyo baada ya kumtuhumu kwa kumteka nyara mtoto kabla ya watu hao kumuua
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/14/131014090950_misri_maandamano_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Vijana wasiokuwa na ajira nchini Morocco na ambao wamefuzu vyuo vikuu wakiitaka serikali kufanya kila iwezalo kubuni nafasi za kazi.  
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/14/131014091452_pich_stop_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Mnamo siku ya Alhamisi mwanamume mmoja anabeba msalaba mjini Pretoria, Afrika Kusini kuhusu mauaji mabaya ya wakulima wazungu.  
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/14/131014091113_jo_burg_car_lights_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Taa za gari hapa zinaonekana karibu na barabara moja nchini Afrika Kusini katika mji wa Johannesburg siku ya Jumatatu. Barabara ambazo hutoza ushuru zimekuwa kaa moto vinywani mwa wanasiasa huku chama rasmi cha upinzani Democratic Alliance kimeweka mabango kwenye barabara ya kutoka Johannesburg hadi Pretoria likiwa na kauli mbiu "ushuru wa barabarani unaletwa kwako na chama tawala ANC
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/14/131014091224_clay_bricks_976x549_bbc_nocredit.jpg
Kijana huyu anatengeza matofali kutoka kwa matope katika kambi ya wakimbizi ya Dadaab. Kambi hiyo ni makao kwa maelfu ya wakimbizi wa Somalia. 
Mwanamitindo hapa amevalia nguo iliyoshonwa na Grace Kelly wa DRC siku ya Ijumaa katika mtaa wa kifahari wa Gombe viungani mwa mji mkuu Kinshasa - wakati wa wiki ya fasheni ya DRC. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/14/131014091302_sa_bishop_976x549_bbc_nocredit.jpg
Mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel Desmond Tutu wa Afrika Kusini alijiunga na watu waliojitolea kusafisha mji wa Cape Town Jumatatu wiki jana wakati alipokuwa anasherehekea miaka 82 ya kuzaliwa kwake.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/14/131014091618_senegal_mats_yousundour_976x549_bbc_nocredit.jpg
Gari hili linalo bango la aliyekuwa waziri wa sanaa nchini Senegal Youssou Ndour ambaye alitupwa nje ya baraza la mawaziri na sasa anajiandaa kurejea kwenye sanaa. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/14/131014090439_prayers_and_water_976x549_bbc_nocredit.jpg
Waumini wa kanisa la Shembe Afrika Kusini wakiwa kwenye maombi siku ya Jumamosi wakiwa wamepiga magoti kwenye ufuo wa bahari mjini Durban ambalo hutembelewa sana na watu wanaopenda michezo ya majini.

Hakuna maoni: