
Majeneza ya watoto waliokuwa miongoni mwa watu waliokufa maji katika kisiwa cha Lampedusa

Mnamo Jumanne vikosi vya usalama katika mji mkuu wa Guinea-Bissau
wanamlinda mwanamume raia wa Nigeria, kutokana na ghadhabu ya raia wa
nchi hiyo baada ya kumtuhumu kwa kumteka nyara mtoto kabla ya watu hao
kumuua

Vijana wasiokuwa na ajira nchini Morocco na ambao wamefuzu vyuo vikuu
wakiitaka serikali kufanya kila iwezalo kubuni nafasi za kazi.

Mnamo siku ya Alhamisi mwanamume mmoja anabeba msalaba mjini Pretoria, Afrika Kusini kuhusu mauaji mabaya ya wakulima wazungu.

Taa za gari hapa zinaonekana karibu na barabara moja nchini Afrika
Kusini katika mji wa Johannesburg siku ya Jumatatu. Barabara ambazo
hutoza ushuru zimekuwa kaa moto vinywani mwa wanasiasa huku chama rasmi
cha upinzani Democratic Alliance kimeweka mabango kwenye barabara ya
kutoka Johannesburg hadi Pretoria likiwa na kauli mbiu "ushuru wa
barabarani unaletwa kwako na chama tawala ANC

Kijana huyu anatengeza matofali kutoka kwa matope katika kambi ya
wakimbizi ya Dadaab. Kambi hiyo ni makao kwa maelfu ya wakimbizi wa
Somalia.
Mwanamitindo hapa amevalia nguo iliyoshonwa na Grace Kelly wa DRC siku
ya Ijumaa katika mtaa wa kifahari wa Gombe viungani mwa mji mkuu
Kinshasa - wakati wa wiki ya fasheni ya DRC.

Mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel Desmond Tutu wa Afrika Kusini
alijiunga na watu waliojitolea kusafisha mji wa Cape Town Jumatatu wiki
jana wakati alipokuwa anasherehekea miaka 82 ya kuzaliwa kwake.

Gari hili linalo bango la aliyekuwa waziri wa sanaa nchini Senegal
Youssou Ndour ambaye alitupwa nje ya baraza la mawaziri na sasa
anajiandaa kurejea kwenye sanaa.

Waumini wa kanisa la Shembe Afrika Kusini wakiwa kwenye maombi siku ya
Jumamosi wakiwa wamepiga magoti kwenye ufuo wa bahari mjini Durban
ambalo hutembelewa sana na watu wanaopenda michezo ya majini.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni