Jumatano, 6 Novemba 2013

WAASI WA M23 SASA WASALIMU AMRI DRC

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/05/131105120527__70910163_70910162.jpg 
Shirika la misaada ya kibinadamu la Umoja wa Mataifa (OCHA) linasema kuwa angalau watu 800,000 wametoroka makwao kufuatia vita kati ya serikali na waasi wa M23. Kundi hilo lilianza harakati zake dhidi ya serikali mwezi Aprili mwaka 2012.  
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/05/131105120555__70912492_70912491.jpg 
Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, inasema kuwa wanajeshi wake wamekomboa ngome mbili za mwisho za waasi wa M23, Tshangu na Runyoni mapema Jumanne.  
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/05/131105120637__70912806_70912805.jpg 
Waasi wa M23 walitoroka maeneo waliyokuwa wameyateka ya sehemu za milimani nchini DRC baada ya jeshi la serikali kukataa ombi la kusitisha vita ili kufanya mazungumzo na serikali na hata kuwaondoa kutoka katika maeneo waliyokuwa wameyadhibiti.  
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/05/131105120608__70912800_70912799.jpg 
Jeshi la Congo liliungwa mkono na wanajeshi wa Umoja wa Mataifa kuwapiga waasi wa M23 Mashariki mwa DRC.  
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/05/131105120540__70910166_70910165.jpg 
Rutshuru ni moja ya maeneo yaliyokombolewa na jeshi la serikali ya DRC, tangu mwishoni mwa wiki  
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/05/131105120652__70913737_70913736.jpg 
Mikoa ya Kivu Kaskazini na Kusini ni maeneo yenye utajiri mkubwa wa madini na yamekuwa kitovu cha mgogoro wa kisiasa ambao umekuwa ukitokota DRC kwa miaka mingi.  

ENDELEA KUWA NASI KWA MATUKIO ZAIDI

Hakuna maoni: