Jumatatu, 4 Novemba 2013

M23 YAWATAKA WAFUASI KUSITISHA MAPIGANO

Wanajeshi wa serikali ya DRC katika vita dhidi ya M23 
Kiongozi wa wapiganaji wa M23 mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo ametangaza kuwa watasitisha mapigano katika vita vyao na jeshi la serikali.

Bertrand Bisimwa alisema kwenye taarifa kwamba anawasihi wapiganaji wote haraka waache uhasama na wanajeshi, ili kuwezesha mazungumzo ya amani kuendelea.

Wanajeshi wa serikali, wakisaidiwa na kikosi cha kuweka amani cha Umoja wa Mataifa, hivi karibuni wamewasukuma nyuma wapiganaji na kuwatoa katika ngome zao nchini.

Mazungumzo ya amani yanafanywa mjini Kampala, Uganda.

Hakuna maoni: