Jumapili, 15 Septemba 2013

HAYA YATAISHA LINI?

Wanajeshi wakivizia wapiganaji wa MNL Zamboanga, Ufilipino
Jeshi la Ufilipino linasema limewazunguka wapiganaji wanaodhibiti mji wa Zamboanga, kusini mwa nchi, baada ya siku sita za mapigano ambayo yamepelekea watu zaidi ya laki saba kuhama makwao.
Mwandishi wa BBC Barani Asia anasema risasi zimekuwa zikifyatuliwa wakati wote huku jeshi likijongelea maeneo mawili ya mwisho yenye mapigano mjini Zamboanga.
Takriban watu 65,000 inajulikana wameuwawa.
Jeshi limeripoti kuwa wengi waliouwawa ni wapiganaji wa kundi la Moro National Liberation Front, MNLF.
Raisi Benigno Aquino na makamu wake wamezuru eneo hilo Jumamosi ili kufanya majadiliano ya kutafuta amani, lakini kwa sasa inaarifiwa wanaongoza jeshi wakati linakabiliana na wapiganaji.

Hakuna maoni: