Malala alipigwa risasi kichwani kwa kutetea haki za wasichana kusoma
Msichana mwenye uraia wa Pakistan ambaye pia ni
mwanaharakati wa elimu , Malala Yousafzai, aliyepigwa risasi kichwani na
wapiganaji wa Taliban, ameshinda tuzo la wanaharakati wa haki za
binadamu la Sakharov ambalo hutolewa na Muungano wa Ulaya.
Malala mwenye umri wa miaka 16 alipigwa risasi mwaka jana kwa kutetea haki za wasichana kupata elimu.
Tuzo la Sakharov hutolewa na bunle la ulaya kila mwaka kwa heshima ya mwanafisikia wa kisovieti Andrei Sakharov.
Mwengine ambaye alioneka kuweza kuipata tuzo
huyi ni Mmarekani Edward Snowden aliyefichua siri ya Marekani kudukua
taarifa za faragha za watu.
Tuzo hiyo ni ya thamani ya dola (65,000) .
Malala alianza kusifika duniani mwaka 2009 baada
ya kuandika blogu kuhusu maisha yake chini ya utawala wa Taliban kwa
niaba ya idhaa ya Urdhu ya BBC,na kuelezea changamoto ya wasichana
kupata elimu nchini humo.
Alikuwa anaishi katika eneo la bonde la SWAT na
jina lake lilikuja kujulikana baada ya jeshi kufurusha wapiganaji kutoka
eneo hilo mwaka 2009.
Kundi la Taliban huwawekea vikwazo sana wanawake
na kukandamiza haki zao na mmoja wa wapiganaji hao alimpiga risasi
alipokuwa ndani ya basi kuelekea nyumbani.
"leo tungependa kueleza dunia kuwa matumaini
yetu yako mikononi mwa vijana kama Malala Yousafzai, '' alisema kiongozi
cha chama cha Ulaya cha conservative Joseph Daul.
Malala alishangiliwa sana kwenye mkutano wa baraza la umoja wa mataifa alipotoa hotuba kusema kuwa kamwe hatanyamazishwa.
Watu wengine ambao wamewahi kupokea tuzo hiyo ni
pamoja na Nelson Mandela wa Afrika Kusini na Aung San Suu Kyi ambaye ni
kiongozi wa upinzani Burma.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni