Ijumaa, 13 Septemba 2013

AFRIKA KATIKA PICHA WIKI HII

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/08/12/130812094722_wiki_hii_picha_976x549_bbc_nocredit.jpg
Katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu, siku hiyo ya Jumanne mtoto akitembea na bunduki bandia kwenye ufuo wa bahari ya Lido
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/08/12/130812095223_wiki_hii_picha_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Mnamo siku ya Jumapili, kijana huyu anaonekana akicheza na mpira katika kambi ya watu walioachwa bila makao kufuatia mapigano katika mkoa wa Kivu Kaskazini karibu na mji wa Goma
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/08/12/130812095442_wiki_hii_picha_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Siku mbili baadaye mama huyu anaanda Ugali katika mji katika kambi nyingine karibu na mji wa Goma
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/08/12/130812095628_wiki_hii_picha_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Mwanamume mmoja Mashariki mwa mji wa Maiduguri Kaskazini Mashariki mwa Nigeria anapuliza ala yake ya muziki wakati wa sherehe za Idd 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/08/12/130812095703_wiki_hii_picha_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Mji wa Maiduguri ni kitovu cha harakati za Boko Haram na hii ndio mara ya kwanza kwa sherehe za idd kufanyika mjini humo tangu kundi hilo kuanza harakati zake
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/08/12/130812095535_wiki_hii_picha_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Mwanamke anawaelekeza vipofu watatu ambao huimba wakati wakiomba pesa katika soko moja mjini Bamako, Mali 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/08/12/130812095041_wiki_hii_picha_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Familia ambazo nyumba zao ziliharibiwa kwenye mafuriko mjini, Khartoum, wanapumuzika kwenye vitanda vyao kando ya barabara Jumanne. Mashirika ya misaada yalisema kuwa watu 11 walifariki na wengine 98,500 wameathiriwa na mafuriko hayo ambayo chanzo chake ni mvua kubwa ambayo imekuwa ikinyesha tangu tarehe moja hadi nne mwezi huu
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/08/12/130812094645_wiki_hii_picha_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Mashua ya uvuvi kwenye ufuo wa bahari katika mji mkuu wa Senegal , Dakar ikielekea baharini siku ya Jumanne ambako boti moja iliharibika na kuvuja mafuta. Hali ingali kudhibitiwa na tayari imezua wasiwasi kuhusu uharibifiu wa mazingira

Hakuna maoni: