Wakimbizi wa ndani nchini Somalia
Maelfu ya watu wanaondoshwa kwa nguvu kutoka kutoka
kambi za muda mjini Mogadishu kutoa nafasi kwa maafisa wa mji huo
kufanya shughuli za usafi na ukarabati.
Hii ni kwa mujibu wa shirika la kimataifa la Amnesty.
Shirika hilo limesema kuwa watu wameendelea
kuondoshwa kwa nguvu, katika miezi ya hivi karibuni licha ya maafisa wa
serikali kukosa kupata maeneo mbadala salama ambako watu hao wanaweza
kuhamia.
“Hili halipaswi kuwa linafanyika kwa watu waliotoroka mji mkuu wakitafuta usalama tena kuhamishwa mkwa nguvu.
Hali hii imesababisha visa vingi vya ukiukwaji wa haki za binadamu.
“Serikali ina wajibu wa kulinda watu hawa
wasiojiweza na kuhakikisha usalama wao,’’ alisema Gemma Davies, mtafiti
mkuu wa shirika hilo la Amnesty International.
Zaidi ya watu 300,000 wanaishi katika kambi za
muda mjini Mogadishu ambako wanajihifadhi kutokana na ukame, njaa na
vita vya miaka mingi nchini Somalia ambavyo vimesababisha vifo vya
maelfu ya watu.
Mnamo mwezi Januari, mwaka 2013, serikali ya
Somalia, ilitangaza mpango wa kuwahamisha maelfu ya wakimbizi wa ndani
kutoka Mogadishu katika kambi zilizo nje ya mji ili kutoa nafasi kwa
ukarabati wa mji huo.
Mpango wa serikali hata hivyo ulionekana kuwa na
dosari ikizingatiwa shughuli yenyewe ya kuwahamisha wakimbizi hao, muda
na eneo salama ambalo wangepelekwa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni