Ijumaa, 13 Septemba 2013

Maji mapya Kenya: Laana au baraka?

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/09/12/130912141813_kenya_maji_1_976x549_bbc_nocredit.jpg
Visima vikubwa vimegunduliwa chini ya ardhi katika eneo kame la Turkana Kaskazini mwa Kenya . Hii ni kwa mujibu wa tangazo la serikali ya nchi hiyo. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/09/12/130912141855_maji_2_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Serikali inakadiria kuwa visima hivyo vilivyopatikana kwa kutumia picha za satelite , huenda vikakidhi mahitaji ya maji kwa nchi nzima kwa kipindi cha miaka sabini.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/09/12/130912141930_maji_3_976x549_bbc_nocredit.jpg
 Watu wa jamii ya Turkana ni watu wa kuhamahama na huathirika mno wakati wa ukosefu wa mvua kwani ina maana kuwa wanakosa maji kwa mifugo wao.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/09/12/130912142343_maji_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Ugunduzi huo wa maji ulitangazwa wakati wa ufunguzi wa kongamano la kimataifa kuhusu maji nchini Kenya lililoandaliwa na shirika la Unesco. Shirika hilo lilishirikiana na serikali ya Kenya pamoja na shirika la maendeleo la Japan JICA
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/09/12/130912142127_maji_6_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Waziri alisema kuwa kipaombele kinapewa mwanzo kukidhi mahitaji ya watu wa eneo hilo. ''Tunatarajia kuwa maji yataweza kupatikana katika kipindi cha mwezi mmoja ujao,'' alisema waziri . 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/09/12/130912142048_maji_5_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Maji hayo pia yatatumiwa kwa kilimo cha unyunyiziaji na viwanda. Hivi maajuzi mafuta yaligunduliwa Turkana na kulifanya eneo hili kuonekana kuwa na utajiri wa rasilimali. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/09/12/130912142011_maji_4_976x549_bbc.jpg
Licha ya rasilimali hizi, wakaazi wa eneo hili wanaishi katika umaskini mkubwa mbali na kuhisi kuwa wametengwa .Wanatarajia kuwa serikali itaweza kuwashirikisha katika uamuzi wa ambavyo rasilimali hizi zinaweza kutumika ili kuwafaidi wakaazi 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/09/12/130912142424_maji_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Wanaharakati wanataka serikali ielewe umuhimu wa kushirikisha wakaazi na kuwapa fursa wao wenyewe kusema ambavyo wanataka rasilimali zao zitumike

Hakuna maoni: